1. Utambulisho na Kukubali Masharti
Kwa kufungua, kutembelea, au kutumia jukwaa la UTALIICHAT, unakubaliana kikamilifu na vigezo na masharti yaliyoainishwa hapa. Ukawa haukubaliani na sehemu yoyote ya masharti haya, hauruhusiwi kuendelea kutumia huduma zetu.
2. Maelezo ya Huduma
UTALIICHAT ni jukwaa linalowaunganisha wazungumzaji wa Kiswahili na watalii pamoja na wanafunzi wa kimataifa wanaotaka kujifunza lugha na utamaduni wa East Africa. Jukwaa hili linatoa fursa kwa watumiaji kujipatia kipato kwa njia ya mazungumzo na mafunzo ya Kiswahili.
3. Usajili na Uamilisho wa Akaunti (Account Activation)
Ili kuanza kutumia huduma zote za mfumo na kuweza kutoa salio lako (Withdrawal) kwenda kwenye mtandao wako wa simu (M-Pesa, Mixx by Yas, Airtel Money au Halopesa), lazima uwe na akaunti iliyothibitishwa na kuamilishwa.
- Ada ya usajili/uamilisho ya TZS 14,500 inalipwa mara moja tu.
- Ada hii inatumika kuhakiki utambulisho wa mtumiaji na kuzuia akaunti za kughushi (spam accounts).
- Ada hii hairudishwa (Non-refundable) mara tu akaunti inapoanzishwa.
4. Mfumo wa Malipo na Kutoa Pesa
Watumiaji wote wanapaswa kuzingatia miongozo ifuatayo kuhusu malipo:
- Salio huongezeka kulingana na idadi ya mazungumzo/jumbe zilizokamilika na mtalii.
- Utoaji wa pesa unachakatwa kwa njia ya Instant Auto-Withdrawal mara tu unapoweka ombi lako.
- Unapaswa kuhakikisha namba ya simu unayotumia kupokea pesa imesajiliwa kwa jina lako sahihi.
5. Mwenendo na Maadili ya Mtumiaji
Watumiaji wote wa UTALIICHAT wanatakiwa kudumisha nidhamu na heshima ya hali ya juu wakati wa kuongea na watalii. Ni marufuku kabisa:
- Kutumia lugha za matusi, ubaguzi au picha zisizo na maadili.
- Kujaribu kumtapeli au kumlaghai mtalii kwa namna yoyote ile.
- Kushiriki taarifa za siri au za kibinafsi zinazoweza kuhatarisha usalama wa mtumiaji mwingine.
Mtu yeyote atakayekiuka miongozo hii akaunti yake itafungiwa mara moja bila taarifa wala kurudishiwa salio lake.
6. Mabadiliko ya Masharti
UTALIICHAT inahifadhi haki ya kubadilisha au kuboresha vigezo na masharti haya wakati wowote ili kukidhi mahitaji ya kisheria na maboresho ya huduma. Mabadiliko yakifanyika yatatangazwa kupitia ukurasa huu.
7. Msaada na Mawasiliano
Ikiwa una swali au changamoto yoyote kuhusu vigezo na masharti haya, unaweza kuwasiliana nasi kupitia Channel yetu rasmi ya WhatsApp au timu ya huduma kwa wateja.